BREAKING NEWS: Taarifa zilizotufikia AJALI mbaya imetokea leo asubuhi majira ya saa mbili asubuhi ikihusisha wanafunzi watano kutoka Chuo cha Mt. Augustino cha jijini Mwanza ambapo msichana pekee aliyekuwepo katika gari hilo kati ya watu watano anaeitwa Beatrice Kwacha amefariki hapohapo katika ajali hiyo iliyotokea eneo la Makuyuni katika barabara ya Arusha-Mwanza.
Watu hao ambao wote ni wanafunzi wa SAUT ambao ni Alex Tarimo, Erick, Evance Mopao na Rowlings John walikuwa katika gari binafsi kutokea Arusha kwa mapumziko ya sikukuu walipata ajali hiyo baada ya Tairi la nyuma la gari hilo kupasuka wakati wakiwa katika mwendo mkali wanne ambao ni wanaume wamejeruhiwa vibaya na wapo hospitali mkoani Arusha.
Taarifa zaidi usikose kutembelea http://www.tzcampusvibe.wordpress.com kupata habari zaidi.
MUNGU AIWEKE ROHO YA MAREHEMU BEATRICE MAHALA PEMA NA AWAPE NGUVU NA AFYA WALE WOTE WALIJERUHIWA.
Amen,pole kwa wafiwa wote wazazi,marafiki na jamii ya saut kwa ujumla.
My condolence 2 Kwacha family
WATA TUMALIZA JAMANI KWAUZEMBE
POLENI SANA WANACHUO KWA MSIBA WA BEATRISE KWACHA MUNGU AILAZE PEMA PEPONI ROHO YA BITRIES AMEN…..! JAMANI TUMEANDAMWA
pole za dhat ziifikie familia ya kwacha. bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe
polen sana wapendwa wanafunzi wa saut bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe aaaaaaaaaaaamen